Sehemu ya Dua na Dhikri mbali mbali

Jawabu: Amesema Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- "Mfano wa yule anayemtaja Mola wake na yule asiyemtaja Mola wake ni mfano wa aliyehai na aliyekufa" Imepokelewa na Al-Bukhaariy
-Hii ni kwa sababu thamani ya maisha ya mtu huwa kulingana na kiwango chake cha kumkumbuka Mwenyezi Mungu Mtukufu.

Jawabu: 1- Humridhisha Arrahman -Mwingi wa rehema-.
2- Humfukuza shetani.
3- Humkinga muislamu kutokana na shari.
4- Hupatikana malipo na thawabu.

Jawabu: "Laa ilaaha illa llaahu" Hapana Mola anayestahiki kuabudiwa kwa haki ila Mwenyezi Mungu. Kaipokea Tirmidhi na bin Majah.

"Al-hamdulillaahi lladhi ah-yaanaa baada maa amaatanaa wailaihin nushuur" Yaani: Kila sifa njema zinamstahiki Mwenyezi Mungu aliyetuhuisha baada ya kutufisha na kwake tutafufuliwa. Wamekubaliana Bukhari na Muslim.

Jawabu: "Alhamdulillaahil ladhi kasaani haadhath thauba warazaqaniihi min ghairi haulin minni walaa quwwatin". Kila sifa njema zinamstahiki Mwenyezi Mungu aliyenivisha nguo hii na akaniruzuku si kwa ujanja wangu wala si kwa nguvu yangu" Imepokelewa na Abuu Daud na Tirmidhiy na wengineo.

Jawabu: "Bismillahi" Kaipokea Imamu Tirmidhiy

Jawabu: "Allaahumma lakal hamdu anta kasautanihi, as aluka khairahu wa khaira maa suni'a lahu, wa audhubika min sharrihi wa sharri maa suni'a lahu" Ewe Mwenyezi Mungu ni zako kila sifa njema, wewe ndiye uliyenivisha nguo hii, ninakuomba mazuri yake na mazuri iliyotengenezewa, na ninajilinda kwako kutokana na shari zake na shari ilizotengenezewa" Imepokelewa na Abudaud na Tirmidhiy.

Jawabu: Utakapoona nguo mpya kwa mwenzako basi unamuombea, na unasema: "Utaimaliza na Allah Mtukufu atakupa badala" Imepokelewa na Abuu Daud

"Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi najilinda kwako kutokana na mashetani wa kiume na mashetani wa kike". Wamekubaliana Bukhari na Muslim.

"Ghufraanaka" Msamaha unatoka kwako. Imepokelewa na Abudaud na Tirmidhiy.

Jawabu: "Bismillahi" Imepokelewa na Abudaud na Tirmidhiy na wengineo.

"Nina shuhudia kuwa hapana Mola anastahiki kuabudiwa kwa haki ila ni Mwenyezi Mungu peke yake hana mshirika, na nina shuhudia kuwa Muhammad ni mja wake na ni mtume wake". Imepokelewa na Imamu Muslim

Jawabu: "Bismillaahi, tawakkaltu alallaahi, walaa haulaa walaa quwwata illaa billah" (Ninatoka) Kwa jina la Mwenyezi Mungu nimemtegemea Mwenyezi Mungu, na wala hakuna ujanja wala nguvu isipokuwa kwa Mwenyezi Mungu. Imepokelewa na Abudaud na Tirmidhiy.

"Bismillah walajinaa, wabismillahi kharajinaa, wa a'laa Rabbinaa tawakkalna" Kwa jina la Mwenyezi Mungu tumerejea, na kwa jina la Mwenyezi Mungu tulitoka, na kwa Mola wetu ndiko tunako tegemea, kisha anawasalimia waliopo ndani. Imepokelewa na Abuu Daud

Jawabu: "Allahummaftahli Ab-waba rahmatika"" Ewe Mwenyezi Mungu nifungulie milango ya rehema zako. Kaipokea Muslim.

Jawabu: "Allaahumma inni as-aluka min fadhlika" Ewe Mwenyezi Mungu ninakuomba katika fadhila zako. Kaipokea Muslim.

Jawabu: Ninasema kama anavyosema muadhini, isipokuwa katika neno: "Hayya a'las swalaa" na "Hayya a'lal falaah" Ninasema: "Laa haulaa walaa quwwata illa billaah" Wamekubaliana Bukhari na Muslim.

Jawabu: Ninamtakia rehema Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake-. Imepokelewa na Imamu Muslim Na ninasema: "Allaahumma rabba haadhihid da'watit taamma, was swalaatul qaaima, aati Muhammadanil wasiilata wal fadhwiila, wab'ath-huu maqaaman mahmuudanil ladhii wa a'ttah". Ewe Mwenyezi Mungu huu ni wito uliotimia, na swala imewadia, mpe Muhammadi wasiila (daraja) na nafasi, na umfufue nafasi nzuri uliyomuahidi. Kaipokea Bukhari.
Na ninaomba dua kati ya adhana na iqaama, kwani dua wakati huo hairejeshwi.

Jawabu: 1- Ninasoma ayatul kursiy: (Itazame katika msahafu) "Mwenyezi Mungu Ndiye Ambaye hakuna yeyote anayestahiki uungu na kuabudiwa isipokuwa Yeye. Ndiye Aliye hai Ambaye Amekusanya maana yote ya uhai mkamilifu unaolingana na utukufu Wake. Ndiye Msimamizi wa kila kitu. Kusinzia hakumshiki wala kulala. Kila kilichoko kwenye mbingu na kilichoko kwenye ardhi ni milki Yake. Na hatajasiri mtu yeyote kuombea mbele Yake isipokuwa kwa ruhusa Yake. Ujuzi Wake umevizunguka vitu vyote vilivyopita, vilivyoko na vitakavyo kuja. Anajua yaliyo mbele ya viumbe katika mambo ambayo yatakuja na yaliyo nyuma yao katika mambo yaliyopita. Na hakuna yeyote, katika viumbe, mwenye kuchungulia chochote katika elimu Yake isipokuwa kadiri ile ambayo Mwenyezi Mungu Amemjulisha na kumuonyesha. Kursiy Yake imeenea kwenye mbingu na ardhi. Kursiy ni mahali pa nyayo za Mola, uliyo mkubwa utukufu Wake, na hakuna ajuwaye namna ilivyo isipokuwa ni Mwenyezi Mungu Aliyetukuka. Wala hakumuelemei Mwenyezi Mungu Aliyetakata kuzitunza. (hizo mbingu na ardhi).Yeye Ndiye Aliye juu ya viumbe Vyake vyote, kwa dhati Yake na sifa Zake, Aliyekusanya sifa za utukufu na kiburi. Aya hii ni aya tukufu zaidi katika Qur’ani, na inaitwa Āyah al- Kursīy." [Suratul Baqara: 255]. 2- Na ninasoma: Bismillaahir rahmanir rahiim. "Sema, ewe Mtume, «Yeye Ndiye Mwenyezi Mungu Aliyepwekeka kwa ustahiki wa kuabudiwa, uumbaji na utakatifu wa Majina na Sifa, Asiye na mshirika katika hayo." "Mwenyezi Mungu ndiye mkusudiwa" (2) «Hakuzaa wala hakuzaliwa" «Wala hakuna yeyote katika viumbe Vyake mwenye kufanana katika Majina Yake, Sifa Zake wala vitendo Vyake.» Mara tatu. "Naanza kusoma Qur’an kwa jina la Mwenyezi Mungu nikiomba msaada Wake. «Allah» ni jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa baraka Mwenye kutukuka, Anayestahiki kuabudiwa na sio mwingine. Nalo ni jina mahsusi zaidi miongoni mwa majina ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, na haitwi kwa jina hili yeyote isipokuwa Yeye Aliyetakasika na sifa za upungufu. «Al-Raḥmān» Mwenye rehema nyingi Ambaye rehema Zake zimewanea viumbe vyote. «Al-Raḥīm» mwenye kuwarehemu Waumini. Na majina mawili haya, kati ya majina ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, yanakusanya uthibitishaji wa sifa ya urehemefu kwa Mwenyezi Mungu Aliyetukuka kama unavyonasibiana na haiba Yake." Sema «Najilinda kwa mola wa mapambazuko". «Kutokana na shari la viumbe na udhia wao" «Na shari ya usiku wenye giza jingi uingiapo na ujikitapo na shari na maudhi mbalimbali yaliyomo ndani yake." «Na shari ya wachawi wenye kupuliza kwenye mafundo wanayoyafunga kwa lengo la kuroga." «Na shari ya hasidi mwenye kuchukia watu, anapowahusudu na kuwadhuru, kwa kutaka neema za Mwenyezi Mungu Alizowaneemesha ziwaondokee.» Mara tatu. "Naanza kusoma Qur’an kwa jina la Mwenyezi Mungu nikiomba msaada Wake. «Allah» ni jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa baraka Mwenye kutukuka, Anayestahiki kuabudiwa na sio mwingine. Nalo ni jina mahsusi zaidi miongoni mwa majina ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, na haitwi kwa jina hili yeyote isipokuwa Yeye Aliyetakasika na sifa za upungufu. «Al-Raḥmān» Mwenye rehema nyingi Ambaye rehema Zake zimewanea viumbe vyote. «Al-Raḥīm» mwenye kuwarehemu Waumini. Na majina mawili haya, kati ya majina ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, yanakusanya uthibitishaji wa sifa ya urehemefu kwa Mwenyezi Mungu Aliyetukuka kama unavyonasibiana na haiba Yake." "Sema, ewe Mtume, «Ninajilinda na kutaka hifadhi kwa Bwana wa watu" "Mfalme wa watu" (2) "Mola wa watu" «Kutokana na udhia wa shetani ambaye hutia watu wasiwasi wanapoghafilika na hujificha atajwapo Mwenyezi Mungu." «Mwenye kupenyeza shari na shaka kwenye vifua vya watu." «Miongoni mwa mashetani wa kijini na kibinadamu.» Mara tatu. 3- "Allaahumma anta rabii Laa ilaaha illaa anta, khalaqtanii wa ana abduka, wa anaa a'laa 'ahdika wawa'dika mastatwa'tu, audhubika min sharri maa swana'tu, abuu u laka bini'matika alaiyya, wa abuu ulaka bidhambii faghfirlii fa innahuu laa yaghfirudh-dhunuuba illaa anta" Tafsiri yake: "Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi ni mja wako, hakuna Mola isipokuwa wewe, umeniumba na mimi ni mja wako, na mimi niko ndani ya ahadi yako, na ahadi yako (ninafanya) kadiri niwezavyo, ninajilinda kwako kutokana na shari ya yale niliyoyafanya, nina kiri kwako kwa neema zako juu yangu, na nina kiri kwako dhambi zangu, nisamehe, kwani hakuna awezaye kusamehe madhambi ila wewe". Imepokelewa na Al-Bukhaariy

Jawabu: "Bismikallaahumma amuutu wa ahya" Yaani: Kwa jina lako Mola wangu ninakufa, na ninakuwa hai. Wamekubaliana Bukhari na Muslim.

Jawabu: "Bismillahi"
Basi ukisahau kuisema mwanzoni mwake basi sema:
"Bismillaahi fii awwalihi wa aakhirihi" Kwa jina la Mwenyezi Mungu mwanzoni mwake na mwishoni mwake. Imepokelewa na Abudaud na Tirmidhiy.

Jawabu: "Alhamdulillaahil ladhi atwa'amanii hadhaa warazaqaniihi min ghairi haulin minni walaa quwwatin". Kila sifa njema zinamstahiki Mwenyezi Mungu aliyenilisha chakula hiki na akaniruzuku si kwa ujanja wangu wala si kwa nguvu yangu" Kaipokea Abuudaudi na bin Maajah na wengineo.

Jawabu: "Allaahumma baarik lahum fii maa razaqtahum, waghfir lahum warhamhum" Ewe Mwenyezi Mungu wabariki katika vile ulivyowaruzuku, na uwasamehe na uwahurumie. Imepokelewa na Imamu Muslim

Jawabu: "Alhamdulillaah" Hakika sifa njema zinamstahiki Mwenyezi Mungu.
3- Na ndugu yake aseme kumwambia ndugu yake: "Yar-hamukallaah" Akuhurumie Mwenyezi Mungu.
Akisema kumwambia hivyo:
Basi naye aseme: "Yah-diikumullaahu wayuslih baalakum" Akuongozeni Mwenyezi Mungu na akutengenezeeni mambo yenu". Imepokelewa na Al-Bukhaariy

"Sub-haanakallaahumma wabihamndika Ash-hadu an laa ilaaha illaa anta Astaghafiruka wa atuubu ilaika. Maana yake " Umetakasika ewe Mwenyezi Mungu, Na sifa njema ni zako, ninashuhudia kuwa hapana Mola ila wewe, ninakuomba msamaha na ninatubia kwako. Imepokelewa na Abuu Daud na Tirmidhiy na wengineo.

Jawabu: Bismillaah Alhamdulillaah. "Sub-haanalladhi sakh khara lanaa haadhaa wamaa kunnaa lahu muqriniina, wa inna ilaa rabbinaa lamunqalibuun" Yaani: «Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu Aliyetudhalilishia (kipando) hiki, na hatukuwa ni wenye uwezo juu yake. Na hakika sisi kwa Mola wetu ni wenye kurejea» Alhamdulillaah, Alhamdulillaah, Alhamdulillaah, Allahu Akbaru Allahu Akbaru, Allahu Akbaru, Sub-haanaka llaahumma inni dhwalamtu nafsi faghfir li fa innahuu laa yaghfirudh dhunuuba illaa anta" Umetakasika ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi nimeidhulumu nafsi yangu nisamehe, kwani hakika hakuna ewezaye kusamehe madhambi isipokuwa wewe. Imepokelewa na Abudaud na Tirmidhiy.

Jawabu: Allahu Akbaru Allahu Akbaru, Allahu Akbaru, "Sub-haanalladhi sakh khara lanaa haadhaa wamaa kunnaa lahu muqriniina, wa inna ilaa rabbinaa lamunqalibuun" Allaahumma inna nas aluka fii safarina haadhaa albirra wattaqwaa waminal amali maa tardhwaa, Allaahumma hawwin a'lainaa safaranaa haadhaa wat-wi anna bu'dahu, Allaahumma antas swaahibu fis safari, wal khaliifatu fil ahli, Allaahumma inni audhubika min wa'thaais safari, waka aabatil mandhwari, wasuuil munqalabi fil maali wal ahli" Maana yake: Mwenyezi Mungu mkubwa, Mwenyezi Mungu mkubwa, Mwenyezi Mungu mkubwa «Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu Aliyetudhalilishia (kipando) hiki, na hatukuwa ni wenye uwezo juu yake. Na hakika sisi kwa Mola wetu ni wenye kurejea» Ewe Mwenyezi Mungu hakika sisi tunakuomba katika safari yetu hii wema na uchamungu, na katika amali zile unazoziridhia, ewe Mwenyezi Mungu turahisishie safari yetu hii na utupunguzie umbali wake, Ewe Mwenyezi Mungu wewe ndiye rafiki katika safari, na ndiye msimamizi katika familia, Ewe Mwenyezi Mungu hakika najilinda kwako kutokana na uchovu wa safari, na mandhari mabaya, na kurejea kubaya katika mali na familia.
Na anaporejea basi atasema maneno hayo, na ataongeza neno:
"Aayibuun, taaibuun, aabiduun, lirabbinaa haamiduun" tumerejea, na tumetubia, na tunamuabudu Mwenyezi Mungu, na kwa Mola wetu ndiko tunakorejesha shukurani. Imepokelewa na Imamu Muslim

Jawabu: "Astaudiukumullaahu lladhii laa tadhwiiu wadaa iu'hu" Maana yake: Nakukabidhini kwa Mwenyezi Mungu ambaye hakipotei alichokitunza. Kaipokea Ahmadi na bin Maaja.

Jawabu: "Astaudiullaaha diinaka, wa amaanataka, wa khawaatiima a'malaka" Maana yake: Ninamkabidhi Mwenyezi Mungu dini yako, na amana yako, na mwisho wa matendo yako. Ameipokea Ahmad na Al- nasaai.

Jawabu: "Laa ilaaha illa llaahu wahdahu laa shariika lahu, lahul mulku walahul hamdu, yuhyii wa yumiitu, wahuwa hayyun laa yamuutu, biyadihil khairi, wahuwa a'laa kulla shai in qadiir" Maana yake: Hapana Mola anaestahiki kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu yeye pekee asiye na mshirika wake, ufalme ni wake na sifa njema ni zake, anahuisha na kufisha, mkononi mwake kuna kheri, naye juu ya kila kitu ni muweza. Kaipokea Tirmidhi na bin Majah

"A'udhubillaahi minash-shaitwanir rajiim" Maana yake: Ninajikinga kwa Allah kutokana na shetani aliye laaniwa. Wamekubaliana Bukhari na Muslim.

"Jazaakallaahu khairan" Allah akuzidishie kheri. Kaipokea Imamu Tirmidhiy

Jawabu: "Bismillahi" Imepokelewa na Abuu Daud

"Al-hamdulillaah lladhii bini'matihi tatimmus swaalihaat": Kila Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu ambaye kwa neema zake hutimia mambo mema. Ameipokea Al Hakim na wengineo.

"Al-hamdulillaahi a'laa kulli haal" Kila Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu kwa kila hali Hadithi iko katika sahihil Jaamii.

Jawabu: Muislamu husema: "Assalaam alaikum warahmatullaahi wabarakaatu" Maana yake: Amani iwe juu yenu na rehema za Mwenyezi Mungu na baraka zake.
Na ndugu yake humjibu:
"Waalaikumussalaam warahmatullahi wabarakaatuh" Na iwe juu yenu Amani na rehema za Mwenyezi Mungu na baraka zake. Ameipokea At-tirmidhiy na Abuu daawod na Ahmad.

"Allaahumma swayyiban naafi'a" (Ewe Mwenyezi Mungu ijaalie Mvua Hiyo ni yenye kupatia na yenye manufaa) Kaipokea Bukhari.

Jawabu: "Mutwirnaa bifadhli llaahi warahmatihi" Tumenyeshelezewa kwa fadhila za Mwenyezi Mungu na rehema zake. Kaipokea Bukhari na Muslim.

"Allahumma innii as aluka khairaha wa audhubika min sharri haa": Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi nakuomba kheri zake na nina jikinga kwako nashari zake. Kaipokea Abuudaud na bin Maajah.

Jawabu: "Sub-haana lladhii yusabbihu rra'du bihamdihi wal Malaaikatu min khiifatihi" Maana yake: Ametakasika yule ambaye radi inamtakasa kwa kumhimidi na Malaika kwa kumuhofu. Muwattwaa Malik.

Jawabu: "Al-hamdulillaahi lladhii aafaani min mab-talaaka bihi, wafadh dhwalanii alaa kathiirin min man khalaqa tafdhwiila" Maana yake: Kila sifa njema zinamstahiki Mwenyezi Mungu aliyenipa afya mimi kwa hili alilompa mtihani huyu, na akanifanya kuwa bora kuliko wengi nakuwa miongoni mwa wale aliowaumba kwa ubora. Kaipokea Imamu Tirmidhiy

Imekuja katika hadithi: "Atakapoona mmoja wenu kwa ndugu yake au kwake mwenyewe, au katika mali yake chenye kumstaajabisha, [Basi na akiombee baraka] kwani kijicho ni kweli (kipo)" Kaipokea Ahmadi na bin Maaja.

"Allaahumma swalli 'alaa Muhammad wa a'laa aali Muhammad, kamaa swallaita 'alaa Ibraahiima wa 'alaa aali Ibrahiima, Innaka hamiidun majiid, Allaahumma baarik 'alaa Muhammad wa 'alaa aali Muhammad kamaa baarakta 'alaa Ibraahiima wa 'alaa aali Ibrahiima, Innaka hamiidun majiid" Maana yake: Ewe Allah shusha rehma juu ya Muhamad na ali zake (familia yake) Muhamad kama ulivyo shusha juu ya Ibrahim na watu wa Ibrahim hakika wewe ni mwenye sifa tukufu, na shusha baraka juu ya Muhamad na watu wa Muhamad kama ulivyo shusha baraka juu ya Ibrahim na watu wa Ibrahim hakika wewe ni mwenye sifa tukufu. Wamekubaliana Bukhari na Muslim.